Skip to main content

Wasikukatishe tamaa watu wanaoonekana kama wana mafanikio huku wakiwa na mwenendo mbaya.

Duniani tunaishi kama tunacheza movie/filamu.Binadamu wamepewa uhusika mbalimbali.Wengine wamepewa uhusika mbaya ili wawaimalishe wale wenye uhusika mzuri.Kwa hiyo mtu anaweza kuwa mbaya lakini akawezeshwa kuwa na uwezo wa mali na nguvu ili kumsukasuka mtu mwema na mtu huyu kujichunguza alipokosa na kumrudia Mungu, lakini yeye huyu mtu mbaya mwisho wake ni mbaya tu.Taifa la Israel kila lilipomkosea Mungu, Mungu aliwainua maadui zao na kuwaonea Israel, si kwamba adui wa Israel walifanya mema na kuinuliwa na Mungu, bali Mungu alitaka kuwarudisha Israel karibu na Mungu.Kweli walipotubu Mungu aliwarudia na kuwashinda adui zao.
Sehemu nyingine mungu anasema usipotenda maagizo yake atakulaani na kukuletea taifa ambalo haliangalii makunyanzi na kukuonea na kula mali ya nchi yako na kukusukasuka mpaka uangamie.Hapa Taifa hili geni linainuliwa kuwa na nguvu na kukuonea si kwamba limetenda mema bali limewekwa katika uhusika mbaya chini ya jua.
Vivyo hivyo kuna watu mmoja mmoja ambao wanakua wamefanikiwa alafu wanatenda mambo mabaya hao wanakua wamewekwa katika uhusika wa watu wabaya chini ya jua , wengine wanaoneka dhahiri wakitumia mali zao kuwaonea watu, watu hawa usiwaige wamewekwa katika uhusika mbaya chini ya jua na miisho yao ni mibaya.

Pia shetani ana watu wake ambao huwapa mali ili kuimarisha utawala wa shetani duniani.Watu wa jinsi hii hufanikiwa lakini uhusika wao ni mbaya kwani hutumia mali walizo nazo kufanya matendo maovu/dhambi yanayoimarisha ufalme wa kishetani duniani.Shetani ana mali tena kimaandiko ni mungu wa dunia.Alimwonyesha Yesu Milki/Mali zake akamwambia ukinisujudia nitakupa milki hizi,Yesu alijua kisheria zilikua za shetani kwani alimdanganya mwanadamu wa kwanza akachukua milki yote aliyokabidhiwa, basi Yesu akamjibu imeandikwa msujudie Bwana Mungu wako na si mwingine.Shetani akamuacha malaika wakaja kumtumikia.Wewe umepataje kazi,mali,tenda kwa kumsujudia shetani kupitia kutoa au kupokea rushwa? Sasa shetani hawezi kuondaka na malaika hawawezi kukutumikia.Kama ulifanya hivyo ulikuwa hujui, tubu kwa Mungu alafu usirudie tena.


Angalia neno hili chini linavyoonyesha jinsi mtu mbaya anavyoweza inuliwa kutumiwa kama fimbo ya laana pale mtu wa Mungu anapokosea.

Kumbukumbu la torati 28:15,49,50,51,52
-15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
-49 BWANA atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;
-50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana;
-51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
-52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa BWANA, Mungu wako.

Basi usiyumbishwe ndugu yangu.Vumilia endelea kufanya mambo mazuri ya kumpendaza usizimie moyo, Mungu atakubarki kwa wakati wake.Endelea kujifunza na kuongeza maarifa, huenda kuna sehemu ndogo sana unakosea.Mungu anasema watu wangu wabaangamia kwa kukosa maarifa.

Comments

Popular posts from this blog

FAIDA LUKUKI UNAZOPATA UNAPOOMBA KILA SIKU. (WHY DAILY PRAYER IS IMPORTANT)

Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1. i-Unapoomba, ahadi za Mungu alizoziahidi kwako zinatimia. Mungu aliahidi atatutupa Roho mtakatifu, lakini Roho mtakatifu alishuka kwa mitume wakiwa katika kuomba siku kumi. Sehemu nyingine Mungu anasema huwapa thawabu wale wamtafutao. Unapoomba upo katika kitendo cha kumtafuta Mungu, kwa hiyo kuna vitu vingine vizuri huwa anakupa ukiwa unaomba hata kama hujaviomba. Kwa hiyo kama huombi hupati ahadi zako.Kwani shetani anakua na nguvu ya kuzivuruga na kuleta vikwazo. Waebrania 11: 6 – “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao”.   ii-Unapoomba ni sawa na binadamu anavyohema kwa kuvuta hewa safi (oxygen) na kutoa nje hewa chafu (cabon), ukiomba unavuta paradiso ndani yako na kutoa nje heeee Dunia, au unamvuta Yesu ndani na kutuoa nje heee ubinadamu.Sasa unapoomba kila siku Y...

KITU KINACHOMUATHIRI BINADAMU KUTOFIKIA MALENGO YAKE.

Nyumba hujengwa kwa hekima (methali 24:3a) Hapa tunajifunza chocote kinachojengwa ili kifanikiwe kinahitaji Hekima, Bila Hekima chochote hakiwezi jengeka vizuri bali kitakuwa kinaharibiwa. Hapa nakuonyesha vitu vichache ambavyo unavijenga ili vifanikiwe vinahitaji Hekima; -Unajenga ndoa (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga watoto wako wawe wacha Mungu, pia wawe watu wazima wajitegemee na wawe msaada katika taifa (Inahitaji Hekima bila hiyo wanaharibika) -Unajenga kampuni, taasisi, biashara, kikundi, kazi, nchi (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga ujirani mwema (Inahitaji Hekima bila hiyo unaharibika) -Unajenga afya yako(Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Kumjenga au kumfundisha mtu kunataka hekima-bila hivyo utamvuruga kabisa. Hiyo ni mifano ya vitu vichache-lakini kumbuka chochote unachofanya unajenga na kinahitaji hekima. Hekima ni muhimu sana katika maisha yetu, mfalme Sulemani alipoambiwa na Mungu omba chochote aliomba Hekima....

SIKU ZOTE PENDA KUTUMIA UZOEFU WAKO.

Daudi alikua kijana mdogo lakini alimuua Goriathi jitu kubwa lililowasumbua sana ndugu zake.Wakati anakwenda kupigana nalo watu wake walimdharau na kuona hawezi.Alipong’ang’ania walimvalisha mavazi yao ya vita, lakini yeye aliyavua akaenda kupambana na goriathi kwa kutumia uzoefu wake, Daudi alitumia kombeo na kweli aliweza kumuangamiza goriathi aliyesumbua sana. Kujifunza ni vizuri lakini changanya na uzoefu wako. -Tumia uzoefu wako katika kuendesha ndoa yako japo umeona unaleta matunda ya kuishi vizuri kwa upendo, umoja na amani. Watu wengi ndoa zao zimeharibiwa kwa kutumia uzoefu wa wengine. Unaweza ambiwa wanaume hawafai au wanawake hawafai kumbe wa kwako anafaa. Mfano- mtu mume wake anaposafiri au mke wake anaposafiri anaweza ambiwa na watu wengine kuwa huko mume wako au mke wako alipo atakua si salama anafanya uasherati-hapo anakuwa anapewa uzoefu na watu wengine ambao sio sahihi. Sasa unakuta shuku mbaya zinamuingia mtu na kuleta chuki kati yao. -Hata katika ulaji kuna ...