Vitu vinavyofanya mungu asisikie maombi yako.hivo hapo chini.Jitahidi
kuvifanya vyote ili mungu akusikie na kukutendea.
1-Kuomba tutumie kwa tamaa zetu.Yakobo 4:3
( Yakobo 4:3- Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba
vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu).
Kumbe naweza omba Imani, vitu vingine vya kimungu, na
mahitaji ya kimwili vibaya, pale ninapopenda nionekane na wanadamu na pia vitu
hivyo visiwe msaada kwa wengine.
2-Maovu na dhambi-Isaya 59:1-2
"1 Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa
wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;
2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na
dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia".
3-Kuvitwaa vinyago na kuviweka moyoni Ezekiel 14:3
(Ezekiel 14:3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na
kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni
laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?) Kuweka moyoni kinyago ni
kupenda kitu zaidi ya Mungu kama mke, watoto, kazi, shule n.k
4-Kutosikiliza kilio cha maskini.Mithali 21:13
"13 Azibaye masikio yake asisikie kilio cha
maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa".
5-Kutosamehe Marko 11:25
(Marko 11:25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni,
mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi
makosa yenu). Maana usiposamehe Mungu hakusamei dhambi naye hasikii wenye
dhambi.
6-Mahusiano mabaya kati ya mume na mke.1 Petro 3:7
(1 petro 3:7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa
akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi
pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe).
7-Kutokuamini Yakobo 1:5-7
"6 Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye
shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na
huku.
7 Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa
Bwana".
8- Kutokaa ndani ya Yesu
na kutoshika maneno yake (Yohana 15:7
Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo
lote nanyi mtatendewa).Kushika maneno maana yake kuyajua na kuyatenda.
9- Kuomba bila kutumia jinan
laYesu.
(Yohana 14:13-14
13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya,
ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
14 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.)
Comments
Post a Comment