MIKOSI inatokana na MAKOSA.Kila unapotapeli au kuiba
fuatilia huwa kuna mikosi/matatizo yanakutokea.Matatizo unayoyapata wakati
mwingine huwa tofauti na kitu ulichoiba au tapeli.unaweza ukakuta umezaa
mlemavu, kansa imeibuka katika mwili wako, umepoteza kiungo, kufa, nyumba
imeungua, gari limeanguka,umenaswa na umeme, unatembea mti unakuangukia,
unateleza bafuni na kupasuka kichwa, nk.Hiyo ni kanuni ya ulimwengu.
Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1. i-Unapoomba, ahadi za Mungu alizoziahidi kwako zinatimia. Mungu aliahidi atatutupa Roho mtakatifu, lakini Roho mtakatifu alishuka kwa mitume wakiwa katika kuomba siku kumi. Sehemu nyingine Mungu anasema huwapa thawabu wale wamtafutao. Unapoomba upo katika kitendo cha kumtafuta Mungu, kwa hiyo kuna vitu vingine vizuri huwa anakupa ukiwa unaomba hata kama hujaviomba. Kwa hiyo kama huombi hupati ahadi zako.Kwani shetani anakua na nguvu ya kuzivuruga na kuleta vikwazo. Waebrania 11: 6 – “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao”. ii-Unapoomba ni sawa na binadamu anavyohema kwa kuvuta hewa safi (oxygen) na kutoa nje hewa chafu (cabon), ukiomba unavuta paradiso ndani yako na kutoa nje heeee Dunia, au unamvuta Yesu ndani na kutuoa nje heee ubinadamu.Sasa unapoomba kila siku Y...
Comments
Post a Comment