Skip to main content

Jinsi ya kuzishinda fikra potofu au mawazo mabaya.

Fikra potofu ni mawazo yoyote yanayokushawishi
kufanya kitu kibaya, mfano kutoongea na mtu fulani, kumchukia mtu, jirani yako au mfanyakazi mwenzako, mwanafunzi mwenzako,
kuiba, kumpiga mtu, kutukana, kuua, kujiua, kudanganya, kusaliti, kuzini, kulewa, kuvuta bangi, n.k.
Jinsi ya kushinda fikra potofu ni kuzikataa, fikra potofu yoyote iambie nakukataa, alafu usiendelee kuwaza kuelekea huko  (mfano fikra inakushawishi kumchukia jirani yako/mafanyakazi /mwanafunzi/mfugaji/ au mfanyabishara mwenzako kwa sababu amekukosea, fikra iambie nakukataa, alafu iambie mimi natakiwa kumpenda jirani yangu hata adui yangu na pia kumsamehe anaye nikosea)

Fikra potofu yoyote ni roho mbaya/roho mbaya maana yake ni roho ya shetani. Fikra potofu au roho mbaya au roho ya shetani usikubaliane nayo kwa kutenda inavyokuelekeza/kukusukuma.Ukikubaliana nayo basi roho hiyo ya shetani hukutawala na kuwa ajenti wa shetani. Roho hiyo itakua inakusukuma kufanya vitu vingi potofu mfano wa vichache nilivyoeleza hapo juu, huo ndio uajenti wa shetani.

Fikra potofu tabia yake kuu ni kuharibu/destroy upande wa pili alafu kuja kukuharibu na wewe pia, sababu unachotenda unajipandia wewe mwenyewe siku zote hukurudia.dunia ni duara, unachotenda huzunguka kukurudia wewe.

Angalizo:Fikra potofu waweza kupewa kupitia mtu mwingine katika maongezi, mtu anaweza ongea ubaya wa mtu Fulani ukajikuta na wewe unamchukia. Jitahidi kuwa makini na watu unaokutana nao au marafiki.
Swali la kirafiki:wewe umeisha wahi kumpanda mtu fikra potofu/mawazo mabaya/roho mbaya, yaani roho ya shetani.
Kama umewahi fanya hivyo, basi tubu kwa Mungu na usirudie tena.


Comments

Popular posts from this blog

FAIDA LUKUKI UNAZOPATA UNAPOOMBA KILA SIKU. (WHY DAILY PRAYER IS IMPORTANT)

Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1. i-Unapoomba, ahadi za Mungu alizoziahidi kwako zinatimia. Mungu aliahidi atatutupa Roho mtakatifu, lakini Roho mtakatifu alishuka kwa mitume wakiwa katika kuomba siku kumi. Sehemu nyingine Mungu anasema huwapa thawabu wale wamtafutao. Unapoomba upo katika kitendo cha kumtafuta Mungu, kwa hiyo kuna vitu vingine vizuri huwa anakupa ukiwa unaomba hata kama hujaviomba. Kwa hiyo kama huombi hupati ahadi zako.Kwani shetani anakua na nguvu ya kuzivuruga na kuleta vikwazo. Waebrania 11: 6 – “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao”.   ii-Unapoomba ni sawa na binadamu anavyohema kwa kuvuta hewa safi (oxygen) na kutoa nje hewa chafu (cabon), ukiomba unavuta paradiso ndani yako na kutoa nje heeee Dunia, au unamvuta Yesu ndani na kutuoa nje heee ubinadamu.Sasa unapoomba kila siku Y...

KITU KINACHOMUATHIRI BINADAMU KUTOFIKIA MALENGO YAKE.

Nyumba hujengwa kwa hekima (methali 24:3a) Hapa tunajifunza chocote kinachojengwa ili kifanikiwe kinahitaji Hekima, Bila Hekima chochote hakiwezi jengeka vizuri bali kitakuwa kinaharibiwa. Hapa nakuonyesha vitu vichache ambavyo unavijenga ili vifanikiwe vinahitaji Hekima; -Unajenga ndoa (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga watoto wako wawe wacha Mungu, pia wawe watu wazima wajitegemee na wawe msaada katika taifa (Inahitaji Hekima bila hiyo wanaharibika) -Unajenga kampuni, taasisi, biashara, kikundi, kazi, nchi (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga ujirani mwema (Inahitaji Hekima bila hiyo unaharibika) -Unajenga afya yako(Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Kumjenga au kumfundisha mtu kunataka hekima-bila hivyo utamvuruga kabisa. Hiyo ni mifano ya vitu vichache-lakini kumbuka chochote unachofanya unajenga na kinahitaji hekima. Hekima ni muhimu sana katika maisha yetu, mfalme Sulemani alipoambiwa na Mungu omba chochote aliomba Hekima....

SHARTI LILILOJIFICHA KWA AJILI YA UPONYAJI WA MWILI WAKO.

  Mungu anataka kukuponya lakini ili akuponye shariti lake ni hili; (Warumi 8: 11…Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu)   Unaona sharti hilo- ameanza na neno “Lakini, ikiwa” maana yake hilo ni sharti yaani ukiwa na Roho aliyemfufua Kristo Yesu yaani Roho wa Mungu au Roho mtakatifu ndani yako ndio utapata uponyaji kamili. Lakini kinyume chake hakuna uponyaji.   Sasa kumbe unahitaji kujua utampataje huyo Roho Mtakatifu na kumtunza kwa faida ya Roho na Mwili wako. Maana yake kama hauna huyo uko hatarini. (i)Tubu dhambi zako zote kwa Mungu-Maana Roho mtakatifu anataka awe yeye mwenyewe tu ndani yako. Moyo wako uwe kama karatasi nyeupe isiyokuwa na doa. (ii)Anza kuishi maisha ya kitakatifu kama kutokua na na chuki, kujiinua, hasira, woga, hofu, dharau, kuwaza mambo mabaya yaliyopi...