Skip to main content

Jinsi ya kijiongezea ubora

Kama bidhaa inavyojengewa ubora,  hata wewe waweza kujijengea ubora, njia ni hii waza mambo mazuri na kujizoeza kuyafanyia kazi.Mawazo ni mbegu zinazokua na kuzaa tabia.Chanzo cha tabia fulani ni mawazo yako, au mawazo unayopewa na kukubaliana kutoka upande wa pili,hii ni kanuni ya dunia.kuanzia sasa anza kuwaza mawazo mazuri kama kuwapenda watu na kuwafanyia mema, waza kuwa jamii niifanyie nini jema, waza kuwa mimi nataka niwe mtu wa kusamehe, waza kuwa mimi nataka niwe jitu moja poleee/baridiii, waza kuwa katika kitengo nilichokuwepo niwasaidie watu bila rushwa, waza kuwa nataka majirani zangu niwapende na kuwasaidia.waza kuwa napenda mke au mume wangu nisimkwaze au kumsaliti kabisa,waza napenda nikipata gari niwape watu lifti, waza napenda nikitukanwa au kuambiwa neno la kuumiza mimi nisijibu pia kwa neno la kuumiza kama kisu/sharp tongue n.k (ukiona uko kinyume na mfano wa mawazo hayo juu machache juo ubora wako kama bidhaa uko chini sana)
Penda kuwaza mawazo mazuri na kujizoeza kuyatende itakuwa tabia na utakuwa umejiongezea ubora. mtu atakapokuita jina lako na ubora wako atauona kuwa mpole, mwaminifu, mwenye huruma, mwenye busara na hekima n.k.haitakiwi jamii ikikuona ione ubaya kama mchelewaji,mvivu chapombe, dakika mbili mbele, malaya,tapeli, mwizi, mzulumishi, mzee wa fitina, mgomvi, n.k.
unapojijingea ubora yale mazuri unayoyafanya ni mbegu kwako, nawe utalipwa mazuri yale yale tena yoliyozidi.unavuna utakachopanda hiyo ni kanuni ya dunia. jiulize unapanda nini sasa, unalofanya sasa lazima lazima lazima likurudie mwenyewe.

Comments

Popular posts from this blog

FAIDA LUKUKI UNAZOPATA UNAPOOMBA KILA SIKU. (WHY DAILY PRAYER IS IMPORTANT)

Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa-Luka 18:1. i-Unapoomba, ahadi za Mungu alizoziahidi kwako zinatimia. Mungu aliahidi atatutupa Roho mtakatifu, lakini Roho mtakatifu alishuka kwa mitume wakiwa katika kuomba siku kumi. Sehemu nyingine Mungu anasema huwapa thawabu wale wamtafutao. Unapoomba upo katika kitendo cha kumtafuta Mungu, kwa hiyo kuna vitu vingine vizuri huwa anakupa ukiwa unaomba hata kama hujaviomba. Kwa hiyo kama huombi hupati ahadi zako.Kwani shetani anakua na nguvu ya kuzivuruga na kuleta vikwazo. Waebrania 11: 6 – “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao”.   ii-Unapoomba ni sawa na binadamu anavyohema kwa kuvuta hewa safi (oxygen) na kutoa nje hewa chafu (cabon), ukiomba unavuta paradiso ndani yako na kutoa nje heeee Dunia, au unamvuta Yesu ndani na kutuoa nje heee ubinadamu.Sasa unapoomba kila siku Y...

SHARTI LILILOJIFICHA KWA AJILI YA UPONYAJI WA MWILI WAKO.

  Mungu anataka kukuponya lakini ili akuponye shariti lake ni hili; (Warumi 8: 11…Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu)   Unaona sharti hilo- ameanza na neno “Lakini, ikiwa” maana yake hilo ni sharti yaani ukiwa na Roho aliyemfufua Kristo Yesu yaani Roho wa Mungu au Roho mtakatifu ndani yako ndio utapata uponyaji kamili. Lakini kinyume chake hakuna uponyaji.   Sasa kumbe unahitaji kujua utampataje huyo Roho Mtakatifu na kumtunza kwa faida ya Roho na Mwili wako. Maana yake kama hauna huyo uko hatarini. (i)Tubu dhambi zako zote kwa Mungu-Maana Roho mtakatifu anataka awe yeye mwenyewe tu ndani yako. Moyo wako uwe kama karatasi nyeupe isiyokuwa na doa. (ii)Anza kuishi maisha ya kitakatifu kama kutokua na na chuki, kujiinua, hasira, woga, hofu, dharau, kuwaza mambo mabaya yaliyopi...

KITU KINACHOMUATHIRI BINADAMU KUTOFIKIA MALENGO YAKE.

Nyumba hujengwa kwa hekima (methali 24:3a) Hapa tunajifunza chocote kinachojengwa ili kifanikiwe kinahitaji Hekima, Bila Hekima chochote hakiwezi jengeka vizuri bali kitakuwa kinaharibiwa. Hapa nakuonyesha vitu vichache ambavyo unavijenga ili vifanikiwe vinahitaji Hekima; -Unajenga ndoa (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga watoto wako wawe wacha Mungu, pia wawe watu wazima wajitegemee na wawe msaada katika taifa (Inahitaji Hekima bila hiyo wanaharibika) -Unajenga kampuni, taasisi, biashara, kikundi, kazi, nchi (Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Unajenga ujirani mwema (Inahitaji Hekima bila hiyo unaharibika) -Unajenga afya yako(Inahitaji Hekima bila hiyo inaharibika) -Kumjenga au kumfundisha mtu kunataka hekima-bila hivyo utamvuruga kabisa. Hiyo ni mifano ya vitu vichache-lakini kumbuka chochote unachofanya unajenga na kinahitaji hekima. Hekima ni muhimu sana katika maisha yetu, mfalme Sulemani alipoambiwa na Mungu omba chochote aliomba Hekima....