Skip to main content

Ujumbe kwa wazazi na Vijana ambao ni wazazi watarajiwa.


(2 Wokorintho 12:14b maana haiwapasi watoto kuweka akiba kwa wazazi, bali wazazi kwa watoto).Hivyo wewe kijana mzazi tarajiwa au ndio umeanza kupata watoto tujipange kuweka akiba kwa watoto wetu tena tusiwe na mawazo ya kuja kuwategemea watoto wetu.
Angalia pia hapo (Mithali 19:14a Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye).
Pia (mithali 13:22 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi) Kumbe inatakiwa kwenda mbele zaidi, tuwe na mipango ya kuwezesha hata wajukuu zetu kurithi kitu kutoka kwetu.

Upande wa Vijana msibweteke kusubiri urithi, neno linasema UTUKUFU wa mwisho utakuwa mkubwa kuliko ule wa kwanza.kama kijana inatakiwa hapo baadae kuja kuwa na mali zaidi ya walizokuwa nazo wazazi  wako, mfano kama ni nyumba/ basi  yako  iwe nzuri kuliko ya wazazi wako, sio kijana unaangalia kanyumba kamoja cha wazazi eti uje urithi.Ukiona kijana mpaka unaelekea utu uzima bado ni tegemezi kwa wazazi jua UNA MATATIZO maana na wewe sasa unaangaliwa uwekeze uwaachie urithi watoto wako na wajukuu zako.(Hagai 2:9a Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema BWANA wa majeshi).

Comments